Mvua iinayoendelea kunyesha ndani na nje ya jiji toka mishale ya saa kumi alfajiri zimezua balaa katika maeneo mengi ya Jiji la Dar es salaam. Mvua hizo zimesababisha baadhi ya mito jijini hapa kufurika huku mitaro ikishindwa kupitisha maji mengi yanayopita kwa kasi swala ambalo limefanya mitaro hiyo kumwaga maji njiani.
Maeneo ya Ubungo Darajani, Kibangu na Riverside yameonekana kujaa maji ambapo maji yamejaa sehemu nyingi ambapo pia maeneo ya Sinza na Tandale pia hayafai kutokana na kujaa kwa maji. Maeneo ya Manzese na Magomeni hasa eneo la Jangwani pia maji yamejaa na kuzuia barabara katika baadhi ya maeneo.
Sio maeneo hayo tu katika maeneo ya Posta, Gongo la mboto, Mbagala na Kurasini pia yamefurika jambo ambalo limesababisha kuwa na foleni kubwa jijini.
Wakazi wa mabondeni hali ni mbaya mno na juhudi za haraka zinahitajika kuwasaidia watu hawa.
Samia: Maneno basi, sasa ni utekelezaji
2 hours ago

No comments:
Post a Comment