Kada wa CCM, Mustafa Sabodo ameahidi kuchimba zaidi ya visima 200 katika majimbo yote ya wabunge wa CHADEMA nchini huku akieleza angependa kuona upinzani unachukua nchi mwaka 2015.
Kada huyo maarufu wa CCM toka enzi za Mwalimu Nyerere alikuwa akipokea mpango wa uchimbaji wa visima hivyo toka kwa Katibu wa CHADEMA Dk. Wilbroad Slaa. Kauli hiyo ya Sabodo ambaye pia aliwasaidia sh100 milioni CHADEMA katika kampeni zao imekuja wakati CCM inakabiliwa na mpasuko kutokana na Siasa za makundi.
Katika mazungumzo hayo Sabodo alimhakikishia Dk Slaa kwamba ataendelea kuisaidia CHADEMA katika miradi mbalimbali inayowahusu wananchi hususani suala la Elimu na maji.
Mabadiliko yanakuja tuongeze nguvu
WASIRA ASISITIZA UMOJA CCM
49 minutes ago

No comments:
Post a Comment