Jana majira ya saa 6:30 mchana katika chuo kikuu mlimani palitokea aibu kubwa ambayo itabaki kumbukumbu. Wanafunzi wa UDSM waliokuwa wameandaliwa kwa ajili ya kuwapokea Marais wawili waliokuwa wageni rasmi katika maadhimisho ya miaka 50 ya kitivo cha sheria chuoni hapo ambao wote ni wahitimu chuoni hapo kwa nyakati tofauti walikumbwa na aibu hiyo.
Mwenyeji wa shughuli hiyo ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya muungano Mh. J.M. Kikwete akiongozana na mgeni mwalikwa ambae ni Rais wa Uganda Yoweri Museveni na Waziri mkuu mstaafu Edward Lowasa na Rais Mstaafu Mzee AlHassan Mwinyi waliingia chuoni hapo mishale ya saa 6 mchana na mara tu baada ya kufika ndipo walipokumbwa na zomeazomea hiyo huku wanafunzi hao wakiimba ' Kama sio juhudi zako Nyerere x 3 mafisadi wangesoma wapi?'.
Naunga mkono swala hilo huku nikianza kukosoa matatizo mbalimbali ambayo serikali inayoongozwa na J.K imeshindwa kuyatatua huku mara nyingi akilalamikia watendaji wake kumkwaza, swali ni je amechukua hatua gani? Hebu jiulize alitegemea kushangiliwa na wanachuo hao kwa lipi? Kama ameshindwa kushughulikia matatizo mbalimbali yanayolikumba Taifa atashangiliwa kwa lipi?
Unawezaje kumshangilia Rais huku unakufa kwa njaa kutokana na mfumuko wa bei na kushuka kwa shilingi? Utamshangiliaje Rais huku Nishati muhimu kwa maendeleo(Umeme) umekuwa haueleweki huku yeye akicheka na wahusika? Unamshangiliaje Rais huku mikopo kwa wanavyuo ikiwa haieleweki na idadi kubwa ya wanaostahili hawapati? Huku baadhi ya vyuo kama Tumaini Dar es Salaam College kikiendelea kutoza ada kubwa mno (2.4million per year) na huduma zikiwa ni mbovu mno, wanafunzi wanasomea chini ya miti, maktaba ikiwa haina vitabu vya kutosha na matatizo ya uhaba wa wakufunzi. Wengi hawapendi kwenda pale ila wanajikuta tayari wamepangwa na bodi ya vyuo TCU Je Rais alitegemea kushangiliwa na watu wenye machungu kama hawa?
Lazima ufike wakati watanzania tuache unafiki na tumpatie kila mtu kile anachostahili, kwa lipi kati ya hayo lingemfanya ashangiliwe? Huku wanafunzi wakishindwa kulipa malipo ya hosteli kutokana na kuchelewa kwa mikopo na wakikabwa koo na mama ntilie mtaani, wana lipi la kufurahia? Nadhani hilo ni funzo tosha na kama mabadiliko yasipofanywa ategemee fedheha kubwa zaidi toka kwa wasomi ambao wanaelewa matatizo chungu nzima ya nchi hii yanayotokana na utawala mbovu.
Unawezaje kuwalipa Dowans 94bn huku Mtanzania wa kawaida akiumia na makali ya maisha kwa uzembe wa watu wawili au watatu walioingia mikataba dhalimu na ya kifisadi? Wanajulikana ila Rais amechukua hatua gani? Ifike wakati tuseme basi, nawapongeza UDSM kwa ujasiri wao na wamefungua njia.
Tuamke Watanzania
WELCOME
MAY GOD BLESS YOU ALL FOR VISITING THIS SITE, A HOPE YOU WILL ENJOY EVERYTHING YOU GET HERE AND IF THERE Z ANYTHING BORING OR SHALLOW LEAVE COMMENTS PLEASE.
BE BLESSED
BE BLESSED
MY DIARY
- RONALDTHEGREAT
- Dar es Salaam, Tanzania, Tanzania
- FRIEND TO EVERYONE AND I BELIEVE EVERYTHING IS POSSIBLE
RONNIE DOCOMENTARY
-
▼
2011
(157)
-
▼
October
(18)
- MAKALI YA MGAO WA UMEME KUREJEA UPYA: WAZIRI WA FE...
- ZITTO AHAMISHIWA ICU:ANA VIJIDUDU 150 VYA MALARIA,...
- BASI LA SUMMRY TOKA DAR-DOM LAPATA AJALI MBAYA, JI...
- WATATU WAFA KWA KIPIGO CHA POLISI DODOMA: NANI ANA...
- NANI ANAWAPA POLISI NGUVU YA KUPIGA RAIA NA KUHARI...
- KILICHOMTOKEA JK UDSM NI HALALI KABISA:NCHI INANUKA
- GHADDAFI ADAIWA KUKAMATWA NA MAJESHI YA NATO
- SHAME: JK AZOMEWA NA WANAFUNZI WA UDSM
- MTANGAZAJI AJITANGAZA SHOGA KWENYE TAARIFA YA HABARI
- USHAURI WA BURE KWA SERIKALI
- MITAMBO MIPYA YA AGGRECO YAPATA HITILAFU KUBWA
- LETS FIGHT AGAINST MALARIA: Miss Mtwara 2011/12 af...
- KADA WA CCM ATAMANI UPINZANI USHINDE MWAKA 2015: A...
- CHRISS BROWN ANG'AA KATIKA BET 2011 AWARDS
- MSHINDI WA BSS APATIKANA
- TUTAFIKA KWELI KWA KAULI ZA VIONGOZI? - Dr H.K Kin...
- CCM WASHINDA KWA TABU iGUNGA Chama Cha Mapind...
- http://www.mwananchi.co.tz/
-
▼
October
(18)
Popular Posts
-
Jana usiku klabu za Chelsea na Real Madrid zilifuata nyayo za Manchester United, Barcelona, Shaktar Donetsk, Inter Milan, Tottenham Hotspu...
-
Jeshi Wananchi la Tanzania limewakamata wanajeshi 20 toka Jamhuri ya Kidemokrasia Ya Congo walioingia nchini kinyume cha sheria. Msemaji wa...
-
Majambazi yaliyokuwa na silaha nzito yamevamia katika kituo cha mafuta cha TOTAL kilichopembeni ya Mlimani City Supermarket na kupora mamili...
-
Timu ya Inter Milan ya nchini Italia imeridhia kumuuza kiungo mshambuliaji wa timu hiyo kwa ada ya £25m. Wesley Sneijder ambae amekuwa akiwi...
-
The Church of England has come out in opposition of members of their clergy consecrating the union of the same sex. The govenment announce ...
-
Klabu ya Manchester United ya England wanajiandaa kuhakikisha wanachukua point zote 3 katika dimba la Emirates siku ya jumapili May 1 ili ku...
-
Usajili uliokamilika kwa timu za Uingereza Everton -Nikica Jelavic toka Rangers Tottenham - Louis Saha toka Everton QPR - Djibril Cis...
-
Chama cha soka nchini Uingereza kimetangaza hukumu ya kumfungia Mchezaji wa Manchester City Mario Baloteli kutokana na kitendo chake cha kum...
-
Kinyang'anyiro cha Urais wa mwaka 2015 umeendelea kuwapa tumbo joto baadhi ya vigogo wa CCM huku kila mmoja akitumia kila njia kuhakikis...
OTHER BLOG LIST
Thursday, October 20, 2011
KILICHOMTOKEA JK UDSM NI HALALI KABISA:NCHI INANUKA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment