Mbunge wa Kigoma Kaskazini Mh Zitto Kabwe jana usiku alihamishiwa katika Kitengo Cha Wagonjwa Wanaohitaji Uangalizi Maalum (ICU) baada ya madaktari kutoridhishwa na hali yake.
Msemaji wa Hosipitali ya Muhimbili(MHN) Jeza Waziri amesema madaktari bingwa waliompima Zitto wamegundua kuwa ana vijidudu 150 vya malaria hali ambayo siyo ya kawaida kwa binadamu na ndio sababu iliyofanya madaktari hao kumhamishia katika kitengo hicho.
Wakati huo huo Spika wa Bunge Anne Makinda baada ya kufika hospitalini hapo na kumjulia hali aliwaambia waandishi wa habari kuwa tatizo la kichwa bado linamsumbua Mh Zitto na serikali inajipanga kumpeleka India kwa matibabu zaidi.
Hali ya mheshimiwa Zitto ilianza kuwa tete mapema wiki hii ambapo aliwahishwa katika Hospitali ya Agha Khan na baadae kuhamishiwa Muhimbili kwa matibabu zaidi, Mh Zitto alipohojiwa alisema kwa kifupi tu "naendelea vizuri" madaktari wamekataza watu mbalimbali kufika hospitalini hapo kuzungumza na Zitto wakiwamo waandishi wa habari.
Wakati huo huo mbunge wa viti maalum (CUF) Claradiana Mwatuka nae amelazwa katika kitengo hicho kutokana na kusumbuliwa na vidonda vya tumbo, mbunge huyo alifikishwa hospitalini hapo jana na hali yake inaendelea vizuri pia.
Tumwombe mungu awaponye viongozi wetu warudi katika majukumu yao ya kitaifa.
WASIRA ASISITIZA UMOJA CCM
52 minutes ago

No comments:
Post a Comment