Kwa mtazamo wangu kwa hali ilivyo sasa katika eneo la Ubungo kutokana na kuwa na mitambo mingi hasa eneo la karibu na darajani ni heri wananchi wa maeneo yale wangehamishwa na kupelekwa maeneo mengine.
Kuna wafanyabiashara ambao hupanga bidhaa zao pembezoni mwa barabara ya Mandela sambamba na Gereji ambayo ipo laribu kabisa na mitambo ya Aggreco ambapo kama litajitokeza tatizo kubwa zaidi ya la leo maisha ya watu wengi yanaweza kupotea, ni zaidi ya mara 6 sasa kwa uzoefu wangu toka nimehamia eneo la Ubungo kwa matatizo kama haya kutokea, au tunasubiri makibwa kama ya MV Spice ndio turekebishe?
Usipoziba ufa..................
WASIRA ASISITIZA UMOJA CCM
50 minutes ago

No comments:
Post a Comment