WELCOME

MAY GOD BLESS YOU ALL FOR VISITING THIS SITE, A HOPE YOU WILL ENJOY EVERYTHING YOU GET HERE AND IF THERE Z ANYTHING BORING OR SHALLOW LEAVE COMMENTS PLEASE.
BE BLESSED

MY DIARY

My photo
Dar es Salaam, Tanzania, Tanzania
FRIEND TO EVERYONE AND I BELIEVE EVERYTHING IS POSSIBLE

Popular Posts

Thursday, October 27, 2011

ZITTO AHAMISHIWA ICU:ANA VIJIDUDU 150 VYA MALARIA, WAJIPANGA KUMPELEKA INDIA

Mbunge wa Kigoma Kaskazini Mh Zitto Kabwe jana usiku alihamishiwa katika Kitengo Cha Wagonjwa Wanaohitaji Uangalizi Maalum (ICU) baada ya madaktari kutoridhishwa na hali yake.
Msemaji wa Hosipitali ya Muhimbili(MHN) Jeza Waziri amesema madaktari bingwa waliompima Zitto wamegundua kuwa ana vijidudu 150 vya malaria hali ambayo siyo ya kawaida kwa binadamu na ndio sababu iliyofanya madaktari hao kumhamishia katika kitengo hicho.
Wakati huo huo Spika wa Bunge Anne Makinda baada ya kufika hospitalini hapo na kumjulia hali aliwaambia waandishi wa habari kuwa tatizo la kichwa bado linamsumbua Mh Zitto na serikali inajipanga kumpeleka India kwa matibabu zaidi.
Hali ya mheshimiwa Zitto ilianza kuwa tete mapema wiki hii ambapo aliwahishwa katika Hospitali ya Agha Khan na baadae kuhamishiwa Muhimbili kwa matibabu zaidi, Mh Zitto alipohojiwa alisema kwa kifupi tu "naendelea vizuri" madaktari wamekataza watu mbalimbali kufika hospitalini hapo kuzungumza na Zitto wakiwamo waandishi wa habari.
Wakati huo huo mbunge wa viti maalum (CUF) Claradiana Mwatuka nae amelazwa katika kitengo hicho kutokana na kusumbuliwa na vidonda vya tumbo, mbunge huyo alifikishwa hospitalini hapo jana na hali yake inaendelea vizuri pia.
Tumwombe mungu awaponye viongozi wetu warudi katika majukumu yao ya kitaifa.

No comments:

Post a Comment