Timu ya Arsenal ya Uingereza inatarajiwa kuvaa jezi yenye jina DUBAI kifuani katika mchezo wa leo usiku wa hatua ya 16 bora katika ligi ya mabingwa Ulaya dhidi ya AC Milan.
Hii inakuja baada ya wote kuwa na mdhamini mmoja ambapo huwa jezi zao zina maandishi ya Fly Emirates kifuani, Arsenal itawabidi kuvaa jezi hizo sababu wapo ugenini. Mara ya mwisho Arsenal kuvaa jezi hizo ilikuwa mwaka 2006 walipocheza na Hamburg ya Ujerumani ambao pia hudhaminiwa na kampuni hiyo ya Uarabuni.
Mchezo wa leo dhidi ya AC Milan utachezwa katika dimba la San Sirro ambapo tayari timu ya Arsenal ipo Italia tayari kwa mchezo utakaochezwa saa 4 na dakika 45 kwa saa za Afrika Mashariki.
SERIKALI KUENDELEA NA UTEKELEZAJI GRIDI YA TAIFA YA MAJI
47 minutes ago
No comments:
Post a Comment