Kwa mujibu wa Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA) haya ndiyo matokeo ya kidato cha nne kwa mwaka 2011 JUMLA YA WATAHINIWA 3671 SAWA NA ASILIMIA 1.09 WAMEPATA DARAJA LA KWANZA JUMLA YA WATAHINIWA 8,112 SAWA ASILIMIA 2.41 WAMEPATA DARAJA LA PILI JUMLA YA WATAHINIWA 21,794 SAWA ASILIMIA 6.48 WAMEPATA DARAJ A LA TATU JUMLA YA WATAHINIWA 146,639 SAWA ASILIMIA 43.60 WAMEPATA DARAJA LA NNE JUMLA YA WATANIHIWA 156,085 SAWA ASILIMIA 46.41 WAMEPATA DARAJA SIFURI Kulingana na taarifa hizi kati ya daraja la 1- 111 ufaulu ni asilimia 9.98 ,Ukilinganisha na wale waliopata kati ya daraja la IV - 0 ambao wamepata asilimia 90.01 Baraza la Mitihani (NECTA) wamekaririwa wakisema kuwa kiwango cha ufaulu kimeongezeka sasa ni wakati wetu wanaharakati wapenda maendeleo ya taifa letu kuyachambua na kuyafanyia tathimini matokeo haya, kisha tuambiane je kiwango cha ufaulu kwa hali hii kinaongezeka au kinapungua. Je hii ndiyo elimu bora nchini Tanzania?
No comments:
Post a Comment