WELCOME

MAY GOD BLESS YOU ALL FOR VISITING THIS SITE, A HOPE YOU WILL ENJOY EVERYTHING YOU GET HERE AND IF THERE Z ANYTHING BORING OR SHALLOW LEAVE COMMENTS PLEASE.
BE BLESSED

MY DIARY

My photo
Dar es Salaam, Tanzania, Tanzania
FRIEND TO EVERYONE AND I BELIEVE EVERYTHING IS POSSIBLE

RONNIE DOCOMENTARY

Popular Posts

Wednesday, February 1, 2012

MASHABIKI 74 WAFARIKI KATIKA FUJO MISRI

Mashabiki 74 wamepoteza maisha yao jana mjini Port Said nchini Misri katika mchezo uliozikutanisha timu za Al Masry dhidi ya timu inayoongoza ligi kuu nchini humo ya Al Ahly ambapo timu hiyo ndogo ya Al Masry ilifanikiwa kuifunga timu ya Al Ahly kwa jumla ya magoli 3 - 1.
Baada ya filimbi ya mwisho mashabiki wa timu mwenyeji ya Al Masry walivamia uwanja na kuanza kuwakimbiza wachezaji wa Al Ahly na kuwapiga ambapo katika fujo hizo wachezaji kadhaa wa Al Ahly walijeruhiwa na Polisi walifanikiwa kuingilia kati na kuwaokoa.
Wengi wa mashabiki hao wamefariki kutokana na kukanyagana na wengine kwa majeraha walipokuwa wakipigana na mashabiki wa timu pinzani.
Rais wa Shirikisho la soka duniani FIFA, Sepp Blatter amesema amesikitishwa sana na tukio hilo ambalo halitegemewi kutokea katika soka mara nyingi na ana majonzi kwa wale waliopoteza ndugu zao kutokana na tukio hilo na kusema kwa kifupi "It was a black day in Footbal"
Chama cha soka nchini humo kimetangaza kusimamisha michezo ligi ya mpira kwa muda usiojulikana wakati huu ambapo uchunguzi unaendelea huku pakiwa na dalili kwa timu ya Al Masry kufutwa katika ulimwengu wa soka.
Mungu aziweke roho za marehemu mahala pema peponi.
Source: SkySports Football Website
www.skysports.com

No comments:

Post a Comment