WELCOME

MAY GOD BLESS YOU ALL FOR VISITING THIS SITE, A HOPE YOU WILL ENJOY EVERYTHING YOU GET HERE AND IF THERE Z ANYTHING BORING OR SHALLOW LEAVE COMMENTS PLEASE.
BE BLESSED

MY DIARY

My photo
Dar es Salaam, Tanzania, Tanzania
FRIEND TO EVERYONE AND I BELIEVE EVERYTHING IS POSSIBLE

RONNIE DOCOMENTARY

Popular Posts

Wednesday, November 2, 2011

NAMBA ZA KUUPIIGIA KURA MLIMA KILIMANJARO ZATOLEWA MUDA WA KUPIGA KURA UKIWA UKINGONI

Hatimaye serikali kupitia Wizara ya Mali Asili na Utalii imetoa namba maalum ambazo zitawawezesha watanzania kuupigia kura mlima Kilimanjaro uweze kuingia katika maajabu mapya saba ya dunia.
Zoezi hilo ambalo lilizinduliwa toka Julai mwaka huu limekuwa la kusuasua na ni baada ya njia pekee ya kuupigia kura mlima huo ikiwa ni kwa njia ya mtandao ambapo ni idadi ndogo tu ya watanzania wenye uwezo wa kufanikisha zoezi hilo kutokana na wengi kutojua jinsi ya kufanya ama kutokuwa na mawasiliano hayo ambayo mara nyingi yanahusisha kompyuta.
Zikiwa zimesalia siku 10 pekee zoezi hilo kukamilika Wizara hiyo imetangaza namba hizo ni 15771 kwa mitandao ya Vodacom, Tigo, Sasatel na Zantel na namba 15021 kwa wateja wa Airtel.
Wazo hilo ambalo katibu wa Wizara hiyo amelipata kwa kijana mdogo ambae hakutaka kumtaja katika mazungumzo yake na waandishi wa Habari jambo ambalo libaonesha viongozi wetu ni wavivu kufikiri. Amesema hadi sasa ni asilimia 20% pekee ya watanzania waliopiga kura huku akihamasisha watanzania kuupigia mlima huo kura za kutosha.
Ili kuweza kupiga kura unatakiwa kutuma neno KILIMANJARO kwenda namba 15771 kwa VODACOM, TIGO, SASATEL & ZANTEL na namba 15021 kwa wateja wa AIRTEL.
Shime Watanzania tuupigie kura mlima wetu kuuingiza katika rekodi hizo.

No comments:

Post a Comment