WELCOME

MAY GOD BLESS YOU ALL FOR VISITING THIS SITE, A HOPE YOU WILL ENJOY EVERYTHING YOU GET HERE AND IF THERE Z ANYTHING BORING OR SHALLOW LEAVE COMMENTS PLEASE.
BE BLESSED

MY DIARY

My photo
Dar es Salaam, Tanzania, Tanzania
FRIEND TO EVERYONE AND I BELIEVE EVERYTHING IS POSSIBLE

RONNIE DOCOMENTARY

Popular Posts

Thursday, November 3, 2011

WAZIRI WA MAMBO YA NJE ATOA KAULI JUU YA MISAADA YENYE MASHARTI YA KUUKUBALI USHOGA.

Waziri wa Mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa Mh. Bernard Membe ametoa kauli ya kupinga kuikubali misaada yenye masharti ya kuzitambua haki za mashoga kama serikali ya Uingereza kupitia waziri wake mkuu David Cameron na Waziri wa mahusiano wa Kimataifa Andrew Mitchel walivyotoa kauli hiyo kwa nchi za Africa huku wakitishia kusitisha misaada kwa nchi zitakazokiuka.
Membe akizungumza na waandishi wa habari mapema leo saa 5 na nusu amesema kamwe Tanzania haiwezi kukubaliana na masharti yaliyotolewa na Serikali ya Uingereza huku akisema watanzania wamezoea kushinda njaa hivyo hata kama wakitunyima misaada yao tutasonga mbele. Kauli hiyo imekuja baada ya jana Rais wa Ghana John Evans Atta Mills akipinga pia masharti hayo moja kwa moja
Aliongeza kwa kusema wiki tatu zilizopita palikuwa na ugeni toka nchini Uingereza ulikuwa ufike hapa nchini ukiongozwa na Balozi ambae amemuoa mwanaume mwenzie na wanaishi kinyumba kama mume na mke na yeye alipofikisha habari hizo kwa Rais alizipinga kabisa japo Balozi wa nchi hiyo hapa nchini akisisitiza ujio huo usingeathiri lolote.
Safi sana Mh. Membe tunataka kauli kama hizi

No comments:

Post a Comment