Serikali ya Uingereza imezitaka nchi zinazoendelea kuzitambua haki za mashoga la sivyo zitapunguziwa ama kuondolewa kabisa misaada inayotolewa na nchi hiyo.
Kauli hiyo kali na yakusikitisha imetolewa na Waziri wa Uingereza anaeshughulikia Maendeleo ya Kimataifa Andrew Mitchel alipokuwa akizungumzia misaada inayotolewa Afrika. namnukuu " We'll cut your aid if you persecute gays". Ametoa kauli hiyo ikiwa tayari serikali yake imeiondolea nchi ya Malawi £19million baada ya kuwahukumu kifungo cha miaka 14 mashoga Tiwangole Chimbalanga 26 na Steven Monjeza 20 waliovalishana pete ya uchumba hadharani.
Waziri huyo pia ametishia kuzipunguzia misaada Uganda inayopata £70million kila mwaka na Ghana £36million toka nchini humo kwakuwa wamekuwa wakipinga ushoga bila woga. Msemaji wa Waziri huyo pia alitoa kauli kali katika kusisitiza hilo akisema " Serikali yetu imejipanga kuhakikisha kuwa vitendo vya kihalifu na unyanyasaji dhidi ya mashoga, wasagaji, watu wenye jinsia mbili na walipandikizwa jinsi tofauti na walizozaliwa nazo vinadhibitiwa na haki zao kutambuliwa katika jamii ndani na nje ya Uingereza" aliendelea kusisitiza akisema "Sasa tutaelekeza misaada yetu kwa wale watakaozingatia hili na tutakuwa tukitoa misaada kila baada ya miezi mitatu na sio kwa mwaka mzima kama ilivyokuwa awali jambo ambalo litatuwezesha kupitia kwa umakini kufuatwa kwa haki hizo. Tutaelekeza misaada ya moja kwa moja pale tutakaporidhika kuwa nchi za Afrika zinafuata masharti yetu ya kupunguza umaskini na kuheshimu haki za binadamu".
Swali linabaki kwetu, Je tupo tayari kuukubali ushoga ili tupatiwe misaada? Tungoje kuona viongozi wetu hasa mkubwa wa nchi kama atatoa kauli kuhusiana na hili. Tayari hapo juzi serikali hiyo ya Uingereza ilitishia kutupunguzia $490million katika bajeti yetu kwa kuwa hatutimizi yale wanayoyataka, hebu wayaainishe basi ili tuelewe. Tuwe makini na tulipinge hili kwa nguvu moja. Shime Watanzania, hii sio sawa mbele za Mungu, tusiogope kutopatiwa misaada.
WELCOME
MAY GOD BLESS YOU ALL FOR VISITING THIS SITE, A HOPE YOU WILL ENJOY EVERYTHING YOU GET HERE AND IF THERE Z ANYTHING BORING OR SHALLOW LEAVE COMMENTS PLEASE.
BE BLESSED
BE BLESSED
MY DIARY
- RONALDTHEGREAT
- Dar es Salaam, Tanzania, Tanzania
- FRIEND TO EVERYONE AND I BELIEVE EVERYTHING IS POSSIBLE
RONNIE DOCOMENTARY
-
▼
2011
(157)
-
▼
November
(29)
- MANCHESTER UNITED WATUPWA NJE:CARLING CUP
- BREAKING NEWS; WANNE WAFA KWA AJALI UBUNGO
- 26th Nov; BAADHI YA WASANII WATAKAOTUMBUIZA ; okoa...
- KUNA UMUHIMU GANI KWA KATIBA YETU KUANDIKWA KWA LU...
- URAIS 2015 WAWACHANGANYA WENGI:TABIRI ZA MASANGOMA...
- HOW TO STOP MASTERBATION ADDICTION
- MOTO MKUBWA WALIPUKA MITAMBO YA UMEME UBUNGO:MITAM...
- BREAKING NEWS: MAFURIKO DAR NA MWANZA
- NCHINI INANUKA:MNADHIMU MKUU WA JWTZ AKAMATWA NA I...
- FROM MOVENPICK TO DAR ES SALAAM SERENA HOTEL:KWELI...
- HIVI NDIVYO ALIVYOLAKIWA PRINCE CHARLES
- POLISI YAWATAWANYA WAFUASI WA CHADEMA ARUSHA
- LADY GAGA ATWAA TUZO 4 ZA MTV EUROPE MUSIC AWARDS
- JESHI LA TANZANIA LAKAMATA WANAJESHI 20 WA CONGO N...
- JESHI LA TANZANIA LAKAMATA WANAJESHI 20 WA CONGO N...
- HUDUMA ZA MAKAMPUNI YA SIMU NCHINI NI MBOVU MNO, T...
- MISS VENEZUELA IVIAN SARCOS ATWAA TAJI LA MISS WOR...
- CHURCH OF ENGLAND OPPOSED TO SAME SEX CIVIL PARTNE...
- EID MUBARAK GREETINGS ALL MUSLIMS: READ THIS
- RAIS KIKWETE AMTEMBELEA VENGU HOSPITALI
- THE MAGICIAN PAGE: KAULI YA DAVID CAMERON YAWAVIMB...
- KAULI YA DAVID CAMERON YAWAVIMBISHA KICHWA MASHOGA TZ
- BALOZI WA UINGEREZA NCHINI AIPINGA KAULI YA MEMBE:...
- MLIMA KILIMANJARO KAMWE HAUWEZI KUSHINDA KWA STAIL...
- WAZIRI WA MAMBO YA NJE ATOA KAULI JUU YA MISAADA Y...
- 2.2 BILIONI ZATUMIKA KUWASOMESHA WATATU TCRA NJE K...
- RAIS WA GHANA AIKATAA MISAADA TOKA UINGEREZA YENYE...
- NAMBA ZA KUUPIIGIA KURA MLIMA KILIMANJARO ZATOLEWA...
- TUNATAKIWA KUUKUBALI USHOGA ILI TUONGEZEWE MISAADA...
-
▼
November
(29)
Popular Posts
-
The 5,000 sq ft home includes a saltwater pool, glassed in sunroom, outside fireplace, 5 bedrooms and 5 baths ... but no apparent grotto,...
-
The Ten Best Gifts for Men to Give Women Le The Ten Best Gifts for Men to Give Women Let's face it; some gifts ...
-
Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma(POAC) imegundua ufisadi wa kutisha uliokuwa unafanyika ndani ya Bodi ya TCRA iliyo chini ya J...
-
Kada wa CCM, Mustafa Sabodo ameahidi kuchimba zaidi ya visima 200 katika majimbo yote ya wabunge wa CHADEMA nchini huku akieleza angependa k...
-
Mapya yaibuka Dowans • Dk. Slaa asema Kikwete anawajua wamiliki wake na Mwandishi wetu WAKATI kampuni ya kuzalisha umeme wa...
-
Naukumbuka wimbo mmoja wa taarab unaimbwa "Jahazi likikosa nahodha chombo huenda mrama". Haya ndiyo yanayoendelea sasa hapa nchini...
-
Johannesburg (CNN) -- South African anti- apartheid icon Nelson Mandela successfully underwent hernia surgery Saturday, a family member told...
-
UTAFITI mpya umebaini kuwa nusu ya wanaume nchini ni wagumba ukipingana madai ya wengi kuwa tatizo hilo linawaathiri zaidi wanawake.Kwa muji...
-
Haya ndiyo baadhi ya yaliyoamuliwa kuhusu madai ya Madaktari Kwa ufupi, kutoka kwa watu waliokuwemo kwenye mkutano wa Madaktari na Waziri Mk...
-
Majambazi yaliyokuwa na silaha nzito yamevamia katika kituo cha mafuta cha TOTAL kilichopembeni ya Mlimani City Supermarket na kupora mamili...
OTHER BLOG LIST
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment