WELCOME

MAY GOD BLESS YOU ALL FOR VISITING THIS SITE, A HOPE YOU WILL ENJOY EVERYTHING YOU GET HERE AND IF THERE Z ANYTHING BORING OR SHALLOW LEAVE COMMENTS PLEASE.
BE BLESSED

MY DIARY

My photo
Dar es Salaam, Tanzania, Tanzania
FRIEND TO EVERYONE AND I BELIEVE EVERYTHING IS POSSIBLE

RONNIE DOCOMENTARY

Popular Posts

Monday, November 14, 2011

BREAKING NEWS: MAFURIKO DAR NA MWANZA

Mvua zinazoendelea kunyesha maeneo mbalimbali nchini zimeanza kuleta athari hasa kwa wakazi wanaoishi maeneo ya mabondeni. Mvua hizo zilizoanza kunyesha mapema mwezi huu athari zake zimeonekana zaidi katika jiji la
Dar es salaam na Mwanza ambapo baadhi ya familia zimekosa makazi kutokana na hali hiyo.

Dar es Salaam
Mvua hizo ambazo zimeanza kunyesha mfululizo kwa siku tatu athari zimeonekana zaidi katika maeneo yenye mifumo mibovu ya upitishaji maji taka. Maeneo kama Tandale kwa Mtogole, kwa tumbo, Shoppers & My FAIR Plaza mikocheni yamezungukwa na maji kabisa jambo ambalo limefanya wanunuzi wanaotumia usafiri wa pikipiki na waenda kwa miguu kufika kwa tabu. Maeneo mengine yaliyokubwa na mafuriko hayo ni Manzese, kimara sambamba na daraja la mlalakuwa katika barabara itokayo Magomeni kuelekea Kawe.

Mwanza
Katika jiji la Mwanza pia mvua hizo zimesababisha maeneo kadhaa katika jiji hilo mfano Nyegezi, Majengo Mapya na Nyamagana kufurika maji na kubwa zaidi ikiwa ni kujaa kwa maji kwa Uwanja wa ndege jambo lililofanya ufungwe kwa muda usiojulikana.
Tahadhari inahitajika kabla ya majanga kama haya na tunaombwa kuwapa msaada wale walioathiriwa na mvua hizi. Mpaka sasa hakuna taarifa yoyote inayoyahusisha mafuriko haya na vifo.

No comments:

Post a Comment